
Chama tawala canada chasaka mrithi wa justin trudeau
Play all audios:

Trudeau alitangaza hatua ya kujiuzulu baada ya kuzidi kupoteza uungwaji mkono ndani ya chama chake na nchini kwa ujumla. Chama cha Kiliberali kinabidi kimtafute kiongozi mpya huku
kikikabiliana na vitisho vya rais mteule wa Marekani Donald Trump vya kuweka ushuru mkubwa dhidi ya bidhaa za kutoka Canada. Soma pia: India, Canada zafukuziana mabalozi katikati mwa mzozo
wa kidiplomasia Kujiuzulu kwa waziri mkuu Trudeau kumekuja miezi kadhaa kabla ya Canada kuingia kwenye uchaguzi. Trudeau mwenye umri wa miaka 53, amesema ataendelea kuwa waziri mkuu hadi
kiongozi mpya wa chama chake atakapochaguliwa.